Monday 31 December 2007

Heri ya Mwaka Mpya

Napenda kuchukua nafasi hii adhimu kuwatikia kila la heri katika kuukaribisha mwaka mpya wa 2008. Mwaka huu tumeona mengi na kukutana na mwengi, yakiwamo ambayo tuliyapenda na ambayo hatokujapenda. Ni vema kuendelea kujaenzi yale yote ambayo tumeweza kujifunza katika mwaka huu. Na ni bora zaidi kuangalia kwa kina kwa yale yote ambayo hatukuweza kuyatekeleza katika mwaka huu, ili tuweze kuyatekeleza katika mwaka ujao.

Zaidi tushereheke kwa amani huku tukiweka mikakati mizuri kwa mwaka ujao.

Monday 5 November 2007

Safarini South Africa

Wapenzi wa kona hii, napenda kuwapa taarifa kuwa nitakuwa safarini South Africa kwa masuala ya kifamilia. Kwa wapenzi wa blog mliopo South napenda kupiga hodi rasni. Kwa muda wote ambao nitakuwepo South nitaendelea na blog hi kwa kuwapa Uhondo,visa na ujumbe wowote ule kuhusu zenj africa ya kusin,

Monday 15 October 2007

Leo ni Sikukuu Zenj (15/10/07)

Wananchi wa Zanzibar leo watendelea kuwepo mapumzikoni, katika kusherekea sikukuu ya Idd El Fitri. Hayo yalitangazwa na Mkurugenzi wa Idara ya Utumishi visiwani humo. Kwa kawaida sikukuu hii huwa na mapumziko ya siku mbili rasmi, hata hivyo mwaka huu iliangukia siku ya mapumziko, hivyo pengine SMZ wakaona ni vema na siku ya Jumatatu wananchi wake waendelee kufaidi kusherekea sikukuu.

Visiwani sikukuu za Idd husherekewa kwa muda wa siku nne mfululizo,ambapo siku mbili kati ya hizo huwa ni mapumziko rasmi, na zingine mbili husherekewa baada ya saa za kazi kwisha. Viwanja rasmi hutengwa na Halmashauri za miji kwa ajili ya watu kwenda huko kushereheka, karibu kila aina ya burudani huwepo katika viwanja hivyo. katika viwanja hivyo huwepo na maduka ya kuuza toys,vibanda vya vyakula, vibanda vya kupiga picha, vibanda vya tombola, vibanda vya taarabu, disco na uchekeshaji na vibanda vingine. Kwa Halmashauri hizo ni wakati mzuri wa kukusanya kodi kubwa katika kipindi kifupi zaidi cha ukusanyaji wa kodi. Aidha kwa wananchi ni wakati wa kutumia kwa nguvu katika kipindi kifupi.

Kwa wafanyakazi wa SMZ sherehe hizi hufana zaidi iwapo zitaangukia mwisho wa mwezi, kwani wengi wao hua na uhakika wa kupeleka familia zao katika viwanja hivyo kwa muda wote. Iwapo una familia, mke/wake na watoto, basi hupenda kuwa na nguo mpya kwa siku zote za sikukuu, pesa ya kwenda na kurudi na za kujichana wawepo viwanjani humo.. huku watoto ukiwa ndio wakati wao wa pekee kununua toys wazipendazo. Hivyo kwa mfanyakazi wa SMZ inabidi awe amejinyima sana ili kuweza kufurahisha familia yake.

Kujinyima kwa wafanyakazi hao si kitu rahisi sana kutokana na viwango vya mishahara na hali halisi ya maisha visiwani humo, hii husababisha wasiwe na mipango ya muda mrefu ya kujiandaa na sherehe hizo, zaidi ya kuomba Mungu sherehe hizo ziangukie karibu na mwisho wa mwezi.

Katika ile awamu ambayo wafanyakazi walikuwa wakilipwa mishahara yao katika siku ya arobaini, kulikuwepo na tabia ya wafanyakazi kulipwa nusu msharaha iwapo sikukuu itaangukia katikati ya mwezi. Hii iliwapunguzia machungu ya kusubiri mshahara wa siku ya arobaini na kuweza angalu kuvinjali na familia zao katika viwanja vya sikukuu. Hata hivyo wakati huu nusu mshahara haikutoka na zaidi leo wameambiwa kuwa wapumzike. Kwa upande wa wengi hii ni kero kwao. Iweje upumzike wakati huna hata senti mfukoni. Wengi wanaona bora wangeenda huko kwenye maofisi yao kufanya kazi kuliko kukaa nyumbani pasipo kuwa na kitu. Mbaya zaidi iwapo mfanyakazi ana akaunti ya katika Benki ya Watu wa Zanzibar(PBZ), ina maana kuwa leo hatoweza kutoa fedha zozote, kwani benki itakuwa imefungwa na PBZ hawana ATM...

Hivyo nina imani kuwa pamoja na nia nzuri ya SMZ, kuwapa wafanyakazi siku ya leo kuwa ya mapumziko, sio wengi ambao wamefurahia tangazo hilo. Zaidi limewaweka katika wakati mgumu wa kujibu maswali mengi toka kwenye familia zao.

Tuesday 9 October 2007

TANZANIA Food and Culture

Na Mwandishi Wetu

TANZANIA imepata fursa pekee miongoni mwa nchi za bara la Afrika, kushiriki Tamasha la Chakula litakalofanyika mwisho wa mwezi huu mjini Conwy, Wales.

Katika taarifa ya mratibu wa tamasha hilo la chakula, Gloria Mutahanamilwa, hiyo itakuwa fursa kwa Tanzania kujitangaza katika nyanja mbalimbali za utali, utamaduni, biashara, uchumi, kilimo, uvuvi na nyinginezo.

"Hili ni tamasha la chakula ambacho ni kitu kinachopewa umuhimu zaidi, lakini tutajumuisha mambo mengine mbalimbali kupitia tamasha hilo, kuna uwezekano wa kufungua njia kwa Tanzania katika kushirikiana na nchi nyingine kupitia nyanja tofauti" alisema mratibu huyo.

Katika tamasha hilo, ujumbe wa Tanzania wa watu takriban 25 pia utahusisha wacheza ngoma, wapiga muziki na wapishi.

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mwanaidi Maajar anaunga mkono jitihada hizi na amethibitisha kuhudhuria tamasha litakaloonyesha vyakula, mapishi, utamaduni na vivutio pamoja na kutoa malelezo kuhusu Tanzania.

Tamasha hilo litafanyika katika mji wa kihistoria wa Conwy uliopo Wales kwa siku mbili yaani Oktoba 27 na 28, mwaka huu na inakadiriwa watu 20,000 toka kona mbalimbali za dunia watahudhuria kwani Conwy ni miongoni mwa miji mikuu ya kihistoria na kitalii.

"Ushiriki wa Tanzania ni wa kujitolea, wajumbe wote wanajitolea lakini bado kuna gharama nyingi ili Tanzania tuwakilishwe ipasavyo," alisema mratibu na kuhimiza watu binafsi na taasisi mbalimbali kuchangia na pia kushiriki.

Taarifa zaidi kuhusu TANZANIA Food and Culture zinapatikana kwenye tovuti yao kwa kubonyeza hapa au kwa kuwasiliana na wandaaji,
Tanzania Centre UK kwa barua pepe tanzaniacentre@hotmail.co.uk au
simu +447745891595.

Tuesday 2 October 2007

Lugha rasmi za SMZ



Hizo hapo juu ndio lugha rasmi zinazotambuliwa na SMZ hapa kisiwani Zanzibar.. Mpangilio unaoonekana hapo juu, ni kutokana na uhumimu wa lugha hizo katika SMZ na wananchi wake kwa ujumla..

Sunday 23 September 2007

stoney stone town

Zanzibar: A drug-fuelled paradise?
Why is it an A list must go destinantion for backpackers ze"vishukas"

Quote:
Originally Posted by Daniel Dickinson

Just a few minutes walk from the winding picturesque alleyways of Zanzibar's historic and much-visited Stone Town is a sight that most tourists will not get to see.
Crouching in small fishing boats and dugout canoes on the shore of Malindi, Stone Town's port are a number of young men injecting themselves with a cocktail of heroin and cocaine.


Tourists come from Europe to sample cheap heroin and cocaine

It is a scene at odds with Zanzibar's image of an exotic beach paradise for well-heeled tourists, but for a growing number of Zanzibaris this is the reality of life on an impoverished island off the coast of Tanzania. Saluum Ibrahim Jiddawi started taking drugs when he was just 15 years old. His reasons for doing so were probably no different from teenagers anywhere in the world; he thought it was cool, his friends were doing it, he was bored at school.

Wasted life

And his life unravelled along predictable lines.
He graduated from smoking cannabis to injecting heroin and over the 15 years of his addiction, lost all his friends, his self-respect, put his family under huge stress and took to stealing and lying to feed his $15-a-day habit, a heavy financial burden on an island where the average wage is less than $1-a-day.


I wasted 15 years of my life, and I regret all the pain I put my family through
Saluum Jiddawi Ex-heroin user

Saluum managed to kick the habit two years ago and now runs an outboard motor repair shop on the Malindi shoreline where addicts remind him on a daily basis of the "biggest mistake" of his life. "I wasted 15 years of my life, and I regret all the pain I put my family through," he said. Saluum was lucky to get out of the drugs scene when he did as the temptation of drugs on the island is as strong as it has ever been.

"Drugs are more available now as Zanzibar is on the international drug routes, but the quality is deteriorating as cocaine and heroin are being mixed with flour." Small packets of foil wrapped brown sugar, as heroin is called locally, is easy to pick up in Malindi for just $1, but because of the poor quality addicts are increasingly injecting rather than smoking it. "Users prefer injecting as the drug goes straight into the blood stream and has a bigger effect," said Saluum.

Spread of HIV

And now addicts are adopting a new technique which is worrying drug abuse specialists. It is called "flash blood".
A user injects heroin, then withdraws a syringe-full of blood which contains a smaller amount of heroin and which is passed to a second user who injects it. The technique means that addicts who cannot afford to buy their own drugs can still get a fix, however diluted. "Such sharing is terribly dangerous," says Dr Steven Nsimba of the Muhimbili University of Health and Allied Sciences.

"It could have devastating consequences for HIV/Aids. If the first person is infected the second person will get a direct transmission of the virus." The prevalence of HIV is under 1% in Zanzibar, well below the 7% on mainland Tanzania, but Dr Nsimba believes that could change. "The spread of HIV could be very fast depending on the number of people who are doing flash blood." No-one knows just how many addicts are using the flash blood technique, although the health authorities in Zanzibar are now trying to gather reliable data.

Drug-fuelled paradise?


Mgeni Hassan from Zayedesa, a local NGO which offers support to addicts, paints a gloomy picture.


Young people do not know what they are doing.

We believe every household in the urban centres has one or two children affected
Mgeni Hassan Zanzibari ngo worker "We are seeing the effects of drug abuse, the increase in crime. Young people do not know what they are doing. We believe every household in the urban centres has one or two children affected." And it seems that Zanzibar may be getting a reputation as a place for drug tourism.
One hotelier, who wants to remain anonymous, said he had met tourists who came from Europe to sample cheap heroin and cocaine. One recent case involving a British tourist ended in tragedy. A 26-year-old man collapsed and died after taking drugs he had bought on the island. Most tourists will, of course, enjoy drug free holidays in Zanzibar and will not be aware of the growing local addiction problem. The authorities on the island are no doubt hoping that Zanzibar never picks up a reputation as a drug-fuelled paradise.


Soma Hapa

Rais alipewa majina ya wauza unga lakini ameyaweka kapuni ni lini atayashughulikia? Hadi vijana wote walewe unga? Taratibu tunaanza kupata sifa ambazo haziendani na U

Thursday 20 September 2007

TV Zanzibar(TVZ): Kuondokana na Analogy kwenda Digital



Luninga ya SMZ imeingia mkataba na serikali ya Japan ambapo, Luninga hiyo itafanyiwa malekebisho ya hali juu toka mfumo wa sasa wa urushaji wa matangazo wa Analogy na kwenda kwenye mfumo wa Digital.

Kwa mjibu wa Mdau hapo juu kwenye picha, matengenezo hayo yanategemea kuanza mapema 2008. Mfumo huu wa digital katika Tanzania upo kwenye TVT, Star TV huku ITV na Channel 10 wakiwa semi digital. Zaidi Wachina nao wamekubaliana na serikali ya mapinduzi zanzibar kuvungua kituo kimpya na cha kisasa zaidi cha Tv. Kituo hicho kinatazamiwa kujengwa katika maeneo ya Masingini. Tv hiyo itakuwa ni full digital na yenye nguvu kubwa zaidi kuliko hiyo ya sasa (TVZ).

Wednesday 19 September 2007

Jumuwata inakuhitaji..


Jumuiya ya Wanablogu wa Tanzania inawakaribisha wanablogu wote katika kuchangia, kurekebisha, kukosoa, kutoa ushauri n.k katika katiba ya jumuiya.

Mchango wako wa kimawazo unahitajika sana ili kuweza kupatikana kwa katiba nzuri kwa manufaa ya wanablogu wote.

Usomapo Tangazo hili tafadhali mjulishe na mwanablogu mwenzako.

Thursday 13 September 2007

Wajane waweka rekodi mpya huko zenj....!

Wajane wa kisiwa cha Zanzibar wameweka rekodi mpya katika fani ya mavazi. Ni baaada ya kuwa wabunifu wa kwanza kupaka/kuchora hinna kwenye vitambaa ambavyo hutumika kutengenezea nguo mbalimbali. Ubunifu huu waliupata kutokana na kuhudhulia kozi ya muda mfupi juu ya kuchora hinna kwenye vitambaa.

Ili lengo la mafunzo hayo liweze kufanikiwa ambalo ni kuongeza kipato kwa Wajane hao, ni muhimu kuona kuwa wanakuwa na sehemu rasmi ya kufanyia biashara zao. Kwa upande huu wa fani zisizo rasmi kuwekuwepo na usumbufu mkubwa wa sehemu za kufanyia shughuli zao, pengine ni kutokana na serikali kutowajali, hivyo kuwasumbu sumbua kila kila.

Sehemu ambayo Wajane hawa na wafanyabiashara wengine katika fani hiyo wamekuwa wakiitumia ni Eneo la mji mkongwe na sehemu ya Uwanja wa Forodhani na baadhi ya mitaa ambayo hutokea katika uwanja wa forodhani kama vile mtaa wa gizenga. Halmashauri ya Mji kupitia maelekezo ya Mamlaka ya Mji Mkongwe, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Maghalibi na ofisi ya Waziri Kiongozi wamekuwa mara kwa mara wakiwaondoa wafanyabiashara hao kwa madai mengi, ambayo mengine uhusisha mambo ya dini.

Kwa kuweza kuweka rekodi ya Dunia, ambapo sasa wataweza kujiongezea mapato yao maradufu, Ni vema kwa serikali kutowasumbua sumbua Wajane hao. Soko lao hilo linawalenga watalii ambao hupatikana katika maeneo ya forodhani ambako kuwa vivutio kadhaa vya Utalii. Na zaidi SMZ sasa iweke mikakati ya kuweza kutambua fani zisizo rasmi, kwani zaidi ya kutoa ajila kwa wahusika zitaweza vilevile kuingiza mapato ndani ya serikali na kusaidia juhudi za serikali kupunguza umaskini kwa wananchi wake.

Ni Msimu wa Beer za Mafichoni...Zanzibar


Mwezi wa Ramadhan huko Zanzibar, hubadilisha sura ya kawaida ya visiwa hivyo, aidha pilikapilika nyingi za kawaida huenda likizo ya muda, huku pilika nyingine huchukua nafasi katika kipindi hiki.

Kwa wanywaji wa bia ambao hawafungi, uungana na wananchi wengine ambao wana imani zingine kuendelea kunywa bia, kwa staili ya kujifungia ndani ya nyumba za ulevi....Kwa ufupi katika kipindi hiki cha mfungo, migahawa, hoteli, baa na majumba mengine yote ya starehe hufungwa. Hakuna sheria rasmi ya kufanya hivyo, ila kwa kuwa imekuwa ikifanyika kwa miaka nenda rudi sasa inaonekana ni kama sheria. Na iwapo ukishikwa unakula mchana katika mfungo huu, basi utasekwa rumande na kuachiwa baada ya siku moja au kushitakiwa kabisa!

Miaka kadhaa huko nyuma Beer ilikuwa ikiuzwa katika hotel za serikali tu wakati wa mfungo huu. Tena waliokuwa wanakusudiwa hapo ni watalii tu...! labda na wageni wa serikali ambao wana imani tofauti. Zaidi ya kuuza bia, hoteli hizo pia ndio zilikuwa zikiuza msosi. Hata hivyo mambo sasa yamechukua sura mpya. Baa nyingi huendelea kufanya kazi katika kipindi hiki, zikiuza bia na misosi. Tofauti ya mwezi huu na miezi mingine ni kuwa unywaji ufanyika kwa kujificha, na katika mazingira ya ukimya kabisa, huku wengi wakisubiri king'ora cha kufuturu...!

King'ora kikisharia, kumbi hizo ufunguliwa milango, redio hufunguliwa na kelele za kawaida za kwenye baa huanza kusikika! Hali hii uwepo kwa muda wa mwezi mzima.

Sunday 9 September 2007

Karibu Kahawa...



Kwa wale waliofika Zenj na kunywa kahawa na kashata mitaani, kahawa hiyo sasa inapatikana kwenye makopo kwa matumizi ya nyumbani.

Friday 7 September 2007

Karume Boys hamna aibu?

Karume Boys imepewa jina hilo baada ya rais wa Zenj kujitosa katika kudhamini mchezo wa mpira wa miguu huko visiwani na hata katika ngazi ya afrika ya mashariki na kati. Rais huyo amekuwa mstari wa mbele kusimamia mchezo huo kwa kuhakikisha kuwa timu za Taifa kama hii ya vijiana wa umri chini ya miaka 17 wanashiriki katika mashindano makubwa.
Kwa kufanya hivyo nina imani kuwa lengo la rais ni kuwajenga vijana hao kimchezo tokea wakiwa vijana ili waje kuingia kwenye timu za wakubwa wakiwa na uzoefu mkubwa katika mchezo huo.

Kilichotokea hivi karibuni huko Burundi, kinatia shaka na kinyaa katika medani ya soka visiwani humo. Kuna tuhuma kuwa vijana hao waliuza mechi kwa jirani zao wa Kenya, ili timu hiyo ya Kenya iweze kuingia hatua ya nusu fainali. Kuuza mechi za kitaifa kwa kweli kunatia shaka sana na kama ni kweli basi itakuwa ni hujuma mbaya kabisa kutokea katika fani hii ya kusakata kabumbu katika visiwa hivyo na hata kwa Tanzania kwa ujumla.

Nikirudi nyuma kuangalia maandalizi ya timu hiyo na safari yake ya Burundi yalikuwa ni ya kusuasua na hasa katika suala zima la gharama za timu hiyo kuanzia kambini kwao hadi nauli ya kwenda huko.

Kuanzia timu za Taifa, hadi kwenye vilabu vya Zenj vimekuwa na tatizo la udhamini, hivyo kufanya kuitegemea zaidi serikali katika kushiriki mashindano ya kimataifa. Rais huyo wa Zenj nina hakika alikubali kuanza kudhamini timu hiyo kutokana na kukosekana kwa wafadhili wenye ridhaa ya SMZ. Kwani sio kila mfadhili hukubalika huko Zenj. Hali ya sasa ya udhamini wa soka, na hata uwezo wa vilabu vya soka huko visiwani ni wa kutia shaka, na hii inadhibitishwa na klabu bingwa ya visiwa hivyo timu ya Miembeni kutaka kujitoa au kuuza nafasi yao ya kushiriki mashindano ya klabu bingwa afrika, kutokana na kukosa fedha za kugharamia maandalizi na ushiriki wa mashindano hayo. Hata yule mfadhili wao ambae aliweza kuwaingiza wapenzi wa Miembeni na watu wengine bure kujaza uwanja wa Amani amejitoa kuidhamini timu hiyo katika mashindano hayo muhimu.

Tatizo kubwa la soka visiwani huko ni kukosekana kwa wafadhili. Kipindi kile cha Mzee Ruska, timu za Zenj zilikuwa zikitamba sana, na ilitokana na kuwa na wafadhili. Kwa mfano timu ya Malindi iliweza kununua wachezaji nyota wa timu ya Taifa ya Zambia, kuchezea timu yao, zaidi waliweza hata kuleta wachezaji toka Ulaya ya Mashariki. Mlandege nayo haikuwa nyuma katika kuwakilisha vizuri visiwa hivyo, ambao wachezaji walikuwa wakilipwa kama ni wachezaji wa kulipwa.

Kuanguka kwa ufadhili wa mtu mmoja mmoja kulifungua ukurasa kwa makampuni makubwa kama ya Bia kuingia katika anga za soka. Hata hivyo SMZ ilipinga vikali udhamini wa makampuni ya Ulevi... Kwa kudai kuwa unakwenda kinyume na maadili ya Nchi. Taratibu vilabu vilianza kudorola na hata kufikia kwa timu ya Taifa.

Kilichotokea huko Burundi kinawezekana kutokana na hali halisi ya maandalizi ya timu hiyo. Inaonekana kuwa timu hiyo haikuwa na motisha wa aina yoyote zaidi ya kushiriki mashindano hayo ili siku ipite na warudi makwao. Timu hiyo inawezekana ilikuwa katika hali ngumu kimaisha huko, kiasi ikiwa ni rahisi kurubuniwa ili kudhibiti njaa zao.

Waziri kiongozi nae aliona hali ngumu ya ufadhili kwa timu hiyo, na kabla ya timu hiyo kwenda huko Burundi alinukuliwa akisikitishwa na wafadhili kutojitokeza kuidhamini timu hiyo. Hayo, pamoja na mengine itakuwa ni busara kusubiri uchunguzi wa ZFA dhidi ya timu hiyo. Aidha itakuwa ni jambo la mbolea kwa ZFA kutujulisha matokeo ya uchunguzi wao. Ambao utatuwezesha kujua kipigo cha magoli matano kilikuwa ni kuzidiwa kimchezo au hujuma!

Monday 3 September 2007

Zenj Watatoa Lini Miss Tz......?



Mshindi wa Miss Tz mwaka huu amewasha moto mkubwa kwa wadau wa urembo wa huko bara, ikiwa ni pamoja na mamiss kadhaa waliopita. Moto huo ambao kuzimika kwake ni songombindo unatokana na madai kuwa miss huyo hana asili ya Utz bara, ukinondoni n.k Usishangae sana kusema Utz bara, kwani huko visiwani hakuna mambo ya Umiss, na nina shangaa huyo mdosi...sori huyo miss kuitwa Miss Tz wakati Warembo wa Zenj hawakushiriki mashindano hayo...

Mara ya mwisho kwa kumbukumbu zangu, warembo wa marashi ya karafuu walishiriki mashindano hayo wakati yakidhaminiwa na fegi za aspen.. sijui bado zipo au la! manake fegi hizo zimeadimika sana mitaani.

Awali ya yote inaonekana kuwa Watz wameshindwa kabisa kuficha makucha yao ya kibaguzi kwa kupiga kelele kwa mdosi huyo mzalendo kutwaa taji hilo. Mimi binafsi sishangai sana, kwani ile dhambi ambayo ipo visiwani huku, imeweza kuvuka bahari na kutua huko Bongo...Tz bara.

Iwapo kungekuwpo na Miss Zenj basi yoyote yule ambae angebahatika kutwaa taji hilo, angechunguzwa kuwa ana asili ya wapi...! Kama ni kutoka kisiwa cha pili basi angeitwa ni mpemba, na iwapo angekuwa anakaa Ng'ambo iliyo karibu na Mji mkongwe basi wangesema ni Mngazija, zaidi iwapo angekuwa na chongo basi moja kwa moja angeitwa ni mnyamwezi( mtu yoyote toka bara).

Utamaduni wa kuangalia mtu ana asili ya wapi upo muda mrefu katika visiwa hivi, kiasi kwamba umeleta kujitenga kimakaazi kwa watu... Tabia hii huko bara haikuwepo huko zamani, lakini sasa naona inaingia kwa kasi kubwa. Sijui inaashiria kitu gani, kwani, huko bara waasia wamekuwa wakishika dhamana kubwa kubwa katika kuongoza nchi pasipo mashaka wala malalamiko yoyote. Leo hii kupatikana kwa miss mdosi wa kitz imekuwa nongwa!

Iwapo tulikuwa tukitembea vifua mbele kupinga ubaguzi wa rangi miaka ile, iweje leo tutoe machozi kwa mtz wa kiasia kutwaa taji la Utz? Au ile dhambi toka Zenj tayali imeshaanza kuingia huko bara? Tuliwahi kuonywa kuwa dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, eti ni sawa na kula nyama ya binadamu, kwani hutoishia kuionja tu, bali utaendelea kuila tu!... Mwakani Watz watahoji ni kwanini Mass wanatoka Kinondoni, au kwa nini wamiss wanatoka katika kabila fulani kila mara... Dhambi hiyo itaendelea tu!

Wazenj mara nyingi wamekuwa wakisoma mifano imara ya Tz bara katika suala zima la kuishi bila kujali huyu anatoka wapi au ana asili ya wapi... Iwapo leo hii mmefikia hatua hii, basi mnapoelekea sio kuzuri kabisa. Mfano wa karibu upo huku visiwani!

Thursday 30 August 2007

Wednesday 29 August 2007

Kauli ya Nahodha ina Walakini

Waziri Kiongozi wa Zenj, ambae yupo mkoani Ruvuma ametoa kauli ya kusisitiza kuwa, Elimu ndio njia pekee ya kuwaletea maendeleo wakazi wa Mkoa huo,kutokana na mkoa huo kukosa Umeme wa kuhaminika na kuwa na barabara mbovu. Msisitizo wa kauli hiyo aliutoa kwa kufananisha ukuaji wa kasi wa uchumi wa Singapore na udodoraji wa maendeleo ya mkoa huo na Tanzania kwa ujumla.

Kauli hii ina utata mkubwa kwani elimu pekee haiwezi kuleta maendeleo yoyote iwapo njia zingine za kuleta maendeleo zitakuwa zimebanwa kwa wananchi. Mkoa wa Ruvuma unasifika kwa kuzalisha Mahindi, Kahawa, Tumbaku,Alizeti na mazao mengine. Kabla ya mwaka 1984, usafiri wa kwenda huko ulitegemea zaidi njia ya anga (ATC).Usafiri wa barabara ulikuwa ni wa usumbufu mkubwa na uliweza kuchukua muda mrefu kufika mkoani. Kufunguliwa kwa barabara ya Makambako - Songea katika kiwango cha lami, kulitoa fursa kubwa kwa mkoa huo kuvuma katika uzalishaji wa Mahindi. Barabara hii haikuja kutokana na elimu ya waakazi wa huko bali ni kutokana na umuhimu mkubwa wa taifa kupata Mahindi na Kahawa toka mkoani huko.

Mkoa wa Ruvuma kwa miaka mingi umekuwa ukitegemea umeme wa nguvu ya jenereta, ambao licha ya kuwa ni ghali kuuendesha, upatakanaji wake umekuwa ni wa kimgao kwa zaidi ya miaka ishirini sasa. Sasa hapa sijui elimu ya aina gani inatakiwa ili mkoa huo uunganishwe kwenye gridi ya taifa, ambayo inapita katika mikoa ya jirani zake.

Nimeshindwa kuelewa kauli ya Nahodha, kati ya kuwa na elimu na uwewezeshaji wa miundo mbinu na uchumi wa mkoa husika. Kwa mfano majumba ya michenzani huko Zenj hayakujengwa kwa kuwa waakazi wa zenj wote walikuwa ni wajuzi wa ujenzi. Yalijengwa kwa sababu uchumi wa Zenj kipindi hicho ulikuwa unaruhusu, na viongozi kwa kushirikiana na wananchi waliona upo umuhimu wa kufanya hivyo.

Kwa mkoa wa Ruvuma kuwaambia kuwa tatizo lao la umeme litatatuka kwa kuwa na elimu na sawa na kuwaondoa njiani tu...

Tuesday 21 August 2007

Wadau



Altune na Kibunango

Umbeya Wenye Manufaa...

Hatua ya mradi wa Usimamizi wa Uhifadhi na Mazingira ya Ukanda wa Pwani "MACEMP" kanda ya Zenj kuanzisha mpango wa kuwafanya wavuvi kuwaripoti kwa siri wavuvi haramu ni mzuri kwa lengo la kuwajua wavuvi haramu. Hatua hii imechukuliwa ili kudhibiti uvuvi haramu ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakiharibu mazingira ya baharini, pamoja na kuhatarisha maisha ya viumbe wa baharani.

Lengo kubwa la mradi huo ni kuhifadhi na kutunza mazingira ya pwani kwa kuondoa umaskini wa wavuvi. Malengo yao kwa kiasi fulani yamefanikiwa kupitia kwa kamati mbalimbali za wavuvi katika kisiwa hicho. Mradi huo umeshatoa boti,ndege,mikopo na nyavu kwa kamati mbalimbali ili kuondoa tatizo la uvuvi haramu huku ikikuza kipato cha wavuvi hao.

Hata hivyo pamoja na utoaji wa vifaa hivyo, tatizo la uvuvi haramu limekuwa likiendelea. Kuendelea kwa tatizo hilo kwa upande mwingine ni kuonyesha kuwa mradi huo bado kuwafikia wadau wote katika sekta ya uvuvi. Zaidi kuna tatizo ndani ya kamati za uvuvi ambao wamelalamikiwa na mradi kwa kuvujisha siri za mikakati ya kudhibiti uvuvi haramu.

Mradi huu ili kuwa endelevu unapaswa kuangalia tena malengo yake, na njia ambazo wanatumia kuwafikia wadau wake. ushirikishwaji wa kamati hizo za uvuvi na wavuvi wenyewe. Iwapo mojawapo wa malengo ni kuondoa umaskini wa wavuvi, hapana shaka basi wawatafutie au kuwaelekeza jinsi ya kupata soko la uvuvi wao(soko la ndani na nje), uhifadhi endelevu wa maeneo yanayotumika kwa uvuvi, maana na athari za uvuvi haramu.
Kutoa vifaa pekee sio njia ya kuweza kufanikisha kuondoa uvuvi haramu na hata umaskini wa wavuvi hao.

Ipo mifano mingi ya miradi ambayo ilipewa vifaa vingi kwa miradi hiyo lakini ikashindwa kuendelea na kuishia kufa baada ya muda mfupi. Hii ilitokana na wadau kutojiona kuwa wapo ndani ya miradi hiyo, na kujenga tabia kuwa maendeleo ya miradi hiyo sio yao bali ni ya serikali au watoa miradi hiyo.

Iwapo mradi wa MACEMP watataka mradi huu uwe endelevu, inawabidi kuangalia ni njia gani ambayo wataweza kuitumia kuhakikisha kuwa wadau wao wanajua umuhimu wa mazingira ya bahari ambalo ndio shamba lao la kuwaingizia kipato. Inawabidi wawafikie hadi wale wavuvi wa chini kabisa,zaidi ya kuishia kwenye kamati na wale wavuvi wanaojulikana huko vijijini. Zaidi ya kuwafikia itawabidi kuwapa elimu tosha ambayo itawafanya wathamini na kutambua umuhimu wa mradi huo kuwa upo kwa ajili ya kuwaondolea umaskini huku mazingira ya bahari na viumbe vyake yakiwa salama.

Sunday 19 August 2007

TV Zanzibar(TVZ): Jionee mwenyewe walivyochoka

Pamoja na kushikilia rekodi ya kuwa kituo cha kwanza cha television ya rangi katika Afrika ya Mashariki kama sio Afrika, Television hiyo imekuwa ikirudi nyuma kimaendeleo kila kukicha. Sababu za kuanguka kimaendeleo zinajulikana sana, kwani zimekuwa zikisikika kila siku masikioni mwetu, toka kwa Viongozi wa Kisiasa hadi kwa Watendaji wa kituo hicho.

Lengo la bandiko hili si kuzungumzia uchakavu wa Majengo au vyombo vya kurushia matangazo ya tv hiyo, bali ni kuzungumzia muundo wa web site yao, ambayo umeniacha hoi bin taabani.

Tovuti ya kituo hicho kikongwe unakatisha tamaa, na haina uhusiano wowote wa moja kwa moja na shughuli za kila siku za kituo hicho. Zaidi Tovuti hiyo ni kama imewekwa kuhifadhi baadhi ya hotuba za Rais na Waziri kiongozi wa Zenj. Pengine ingependeza zaidi iwapo tovuti hiyo ingekuwa ni ya Ikulu au ya Ofisi ya WK!

Sijui ni kazi ya Mkurugenzi au Afisa Uhusiano au Mwangalizi wa ofisi kusimamia update za tovuti hiyo. Kwa yoyote ambae anahusika basi ameshindwa kabisa kuelewa ni kwa nini TV huwa na tovuti, au ndio hadithi ile ile ya vyombo vya SMZ kujipendekeza zaidi kwenye Ofisi za Wakubwa wao, na kusahu kushughulikia maendeleo ya Ofisi zao!

Kwa ufupi ni aibu kubwa na ni kituko kikubwa kama si kioja kwa TVZ kuiweka hewani tovuti yao. Kama walikuwa hawajawa tayali kuweka tovuti, wangeweza tu kushikiria domain yao bila ya kuirusha hewani kitu ambacho hakina uhusiano wowote na shughuli zao za kiutendaji, hata historia yao. Zaidi hiyo Elimu kwa Televisheni naona bado kufikiwa au kufanyiwa kazi

Wednesday 15 August 2007

Mbinu za Kizenj za Kusafirisha Mizigo...



Moja ya mambo niliyo yaona huko UK ni jinsi wazenj wanavyojitahidi kusafirisha malundo ya vitu vilivyotumika toka UK kwenda Zenj... Mazagazaga hayo ni kuanzia mafriji, mavideo(VHS), maprinter, mamonitor, makomputer, majiko ya umeme /gasi mabafu, vyoo, n.k.




Makontena ya size ya futi 40 ndio maalufu katika kusafirishia mazagazaga hayo.. ambayo mengine yapo katika hali mbaya sana kutumika zaidi ya kufaa kwa kutupwa tu.



Leo hii tuangalie jinsi ya kusafirisha magari matano katika kontena la futi 40......






















Wednesday 8 August 2007

Safarini Suomi...

Baada ya kuona Vituko kibao vya wazenj hapa Uk... takribani kwa miezi minne sasa, Nageuza safari na kurudi kijiweni huku nikiwa na rundo la vituko vya wazenj hapa uk... tokea wazungu wa unga, hadi vitangi, wasomi na wafanyabiashara, wazazi hadi wajane... ili mradi ni vituko kede kede.. nikipata nafasi nitakuwa nawapasha baadhi ya vituko vyao...

Thursday 14 June 2007

Mahakama Kuu ni Kimeo....

Nimewahi kuandika kuhusu mashaka makubwa ya mahakama za zenj katika mabandiko yaliyopita, leo hii kumeibuka kadhia nyingine ambayo hapana shaka ipo kwa muda mrefu tu huko zenj..

Imeripotiwa kuwa mahakama za zenj, hasa Mahakama Kuu haina majaji wa kutosha hivyo kukosa hadhi ya kuitwa Mahakama Kuu kwa mujibu wa katiba ya visiwa hivyo. Tatizo la Majaji huko visiwani lipo kwa muda mrefu sana, ingawa kuna wakati smz ilijitia kifua mbele kwa kukodisha majaji toka nje ya visiwa hivyo(Mapopo).

Kwa mwananchi wa kawaida hawezi kuamini kuwa Visiwa hivyo havina majaji, kwani wao mtu yoyote afanyae kazi mahakamani basi ni jaji, kama ilivyokuwa katika hospitali zao kwa wafanyakazi wote huitwa ni madokta.

Pengine ujuha huu wa kushindwa kutofautisha mgawanyiko wa ngazi za wafanyakazi, upo ndani ya vibosile wa SMZ kiasi cha kujisahau kuwa hawana Majaji wa kutosha kuendesha kesi lukuki katika Mahakama Kuu. Udhaifu wa mahakama za zenj na hasa katika watendaji wake umekuwa ni gumzo kubwa katika kipindi hiki, wakati kuna fufunu ya uteuzi wa Jaji Mkuu mpya wa Tanzania,

Ukiachana na hayo ambayo yanatia kichefuchefu, Mahakama ya Mkoa wa Mjini Magharibi ina Mahakimu watatu tu, ambao kwa maneno mengine ndio Mahakimu wa Mikoa yote ya Zanzibar! kwani sio siri kuwa sijawahi kusikia Hakimu wa Mikoa mengine minne wakitajwa, licha ya kesi walizohukumu kuripotiwa...! Hao Mahakimu wa wilaya wapo kwa hesabu ya vidole, na wengi wao wapo katika Mahakama za wilaya ya Mjini na ile ya Magharibi... Nasikia huko Pemba kuna mahakama ya Mkoa vilevile, hata hivyo Hakimu wake kutwa yupo Vuga!

SmZ kupitia kwa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali wanapaswa kuja na suluhisho la kudumu kuhusu kadhia hii, na sio kila siku kuwa ni watetezi wa uchovu wa SMZ. Iwapo wao ndio wanasimamia Mahakama na sheria zake, basi hawana budi kuwa na mipango madhubuti ili kuona kuwa vyombo vya haki visiwani humu vimekamilika kwa mujibu wa sheria na katiba ya visiwa hivyo. Kitendo cha kuwaondoa Wapopo katika Mahakama zetu kilikuwa kizuri kwa manufaa ya watu na uchumi wetu unaodorola, aidha ipo haja basi ya ofisi hiyo kupanda Jahazi hadi bara ili kupata Majaji wenye kujua sheria zetu na maadali ya Mtanzania.

Friday 8 June 2007

'Ongezeko la Uzaaji UK' Wazenj Hawako Nyuma....

Imeripotiwa kuwa kumekuwepo na ongezeko kubwa la uzaaji hapa UK, ikiwa ni ongezeko kubwa kwa miaka 26. Ongezeko hilo la uzaaji, limechangiwa na wahamiaji miongoni mwao wakiwa ni wazenj.

Moja kati ya watoto watano wanaozaliwa hapa, amezaliwa na mhamiaji, hivyo kufanya ongezeko la asilimia kumi kwa mwaka kwa watoto wanaozaliwa na wahamiaji. Mwaka 2006 walizaliwa watoto 669,531 kwa wastani wa kila mzazi wa 1.87 huku wahamiaji wakizaa asilimia 21.9 ya watoto wote waliozaliwa mwaka 2006. Wahamiaji wengi ni kutoka nchi za ulaya ya mashariki, wengi wao wakiwa ni Wapoland. Zaidi kumekuwepo na ongezeko kubwa watoto toka kwa wanawake wa Pakistan, India, Afrika na Mashariki ya Kati. Wachunguzi wa mambo wanasema tokea mwaka 1997 (labour ilipoingia madarakani) kiasi cha wahamiaji milioni 1.5 wamehamia UK.[1]

Wanawake wengi toka Zenj hawapo nyuma katika suala la uzaaji, wengi wa wanawake hao ni kinamama wa nyumbani. Nilipojaribu kuulizia zaidi kuhusu uzaaji huo wa kasi, wengi wao walisema ni kutokana na mafao mazuri ambayo hutolewa na serikali ya hapa, hivyo kutokuwa na wasiwasi juu ya malezi na usomeshaji wa watoto hao tofauti na kama ingekuwa huko Zanzibar, ambapo jukumu lote lipo kwa mzazi pekee..!



1.Source: Daily Mail, June 8 2007.

Saturday 19 May 2007

Madeleine wa Zenj

Wengi wetu sasa tunajua kutoweka kwa Madeleine, mtoto wa miaka minne, raia wa Uingereza aliyetoroshwa huko Ureno yapata siku kumi na sita sasa. Vyombo vya habari na hasa vya hapa UK vimekuwa vikitoa maendeleo ya sakata hilo katika kila habari zao. Hivyo kuweza kuwafikia watu wengi kadiri iwezekanavyo. Leo wakati Fainali ya Kombe la FA, kati ya Man Utd na Chelsea, video ya dakika nne ya Madeleine inategemewa kuonyeshwa.Hivyo kuweza kutazamwa na watu zaidi ya nusu bilioni duniani kote.

Huko Zenj kuna mtoto wa kike wa miaka kumi na sita ameripotiwa kutoroshwa na mwalimu wake yapata miezi mitatu sasa. Jeshi la polisi visiwani humo limeomba kusaidiwa na jeshi la polisi la kimataifa(interpol) katika kumtafuta mtoto ambae jina lake ni Maryam Farid Said.

Tofauti ya Maryam na Madeleine ni kubwa sana, Madeleine ni mtoto mdogo sana asiejua hili na lile, wakati Maryam ni msichana mkubwa ambae anajua nini anafanya. Cha kusisimua zaidi ni kuwa Maryam hii ni mara yake ya pili kutoroshwa na wanaume.

Msichana huyo ambae alikuwa ni mwanafunzi wa shule ya binafsi ya bweni huko Bububu Zanzibar ana undugu na Rais wa Tanzania Jakaya M. Kikwete hivyo kuweka utoroshwaji wake kuwa wa mvuto zaidi. Polisi wa visiwani hapo wanashuku kuwa mtoto huyo atakuwa ametoroshwa na mwalimu wake ambae ni raia wa Uganda.

Iwapo mtoto huyo akipatikana, wazazi wake ambao sasa wanamtafuta, itabidi wamkalishe kikao mtoto huyo, kwani hii ni mara ya pili kutoroshwa hivyo kujenga hofu juu ya tabia yake kwa ujumla. Hapana shaka kuwa mtoto huyo anashirikiana na hao wanao mtorosha hivyo kufanya utafutaji wake kuwa mgumu zaidi. Zaidi nawatakia kila la heri Wazazi wa mtoto huyo katika jitihada za kumtafuta mwanao. Hali kadhalika wanachi ambao kwa namna moja ama nyingine ambao watakuwa na habari yoyote ya kuweza kupatika kwa mshichana huyo watoe ushirikiano wao kwa kutoa taarifa katika vyombo husika.

Wednesday 16 May 2007

Wazenj wa UK na Vituko Vyao...

Nilipofika hapa UK yapata mwezi sasa, nilikuwa na hamu kubwa ya kukutana na watz wanaishi huku, zaidi kuonana wa Wazenj wa huku ili niweze kubadilishana nao mawazo kuhusu vituko, vioja na kadhia kadha wa kadha za huko Zenj.
Well haikuwa kazi kubwa kabisa kuwatafuta wazenj, kwani nilipofika mwenyeji wangu alikuwa ametingwa sana na kazi zake za kila siku, hivyo alinitaka radhi kuwa hataweza kunipikia chakula cha jioni. "nikahisi sasa ndio kuna kulala na njaa" Hata hivyo alinitoa hofu kuhusu kupata kwa msosi, kwa kuniambia kuwa tayali ameshatoa oda ya msosi, ambao anahisi kuwa utanifaa na kunikumbusha huko bongo, na hasa katika soko la usiku la chakula huko Zenj(Forodhani).
Muda si mrefu tokea kuingia ndani kwa mwenyeji wangu, chakula cha jioni kikaletwa! MMhm nikaamini maneno yake, kwani ulikuwa ni msosi ambao nimeukasa kwa muda mrefu sasa... Chapati, samaki waliokaangwa kwa viuongo rukuki vya kisiwani, mchuzi mzito maandanzi, na mazagazaga mengine kibao.. ile harufu yake ilipofika puani mwangu, mate kibao yalijaa mdomoni. Baada ya kufakamia msosi ule wa jioni, mwenyeji wangu aliniambia kuwa umetoka kwa Wazenj ambao wao wamefungua mgahawa bubu wa kupika vyakula kwa order.
Asubuhi yake niliamua kuingia mitaani kuangalia hili na lile, baada ya kutembea tembea bila dira maalumu nilijikuta naingia kwenye sehemu ya kukatia nywele. Hapo niliamua kupunguza nywele zangu. Hata hivyo kulikuwa na watu wengi, hivyo nikabidi kusubiri. Vinyozi walikuwa kama wanne hivi wakiendelea na kazi zao... baadae walianza kuongea kwa lugha ya kiswahili yenye rafudhi ya mwambao, nikahisi hapana shaka watakuwa ni Wazenj, hivyo nikajiweka sawa kuwasikiliza. Hata nafasi ya kunyolewa ilipopatikana nilikaribishwa kwa lugha ya Kiingereza... mimi nikajibu kwa lugha ya Kiswahili. Nikanyolewa huku tukiongea hili na lile na hasa mambo ya Zenj. Nilipomaliza nikawauliza sehemu ambayo ninaweza kukutana na Watz wengi kwa wakati mmoja. Wakanielekeza.
Ni jioni, nikaamua kwenda kutembelea sehemu ambayo nitakutana wa Watz wengi kwa wakati mmoja. Ni baa maridadi kabisa na ya kisasa. Nilipoingia ndani ilikuwa imejaa watu kibao wa kila rangi. Baa ya kuchukua bia yangu, nikaanza kutafuta sehemu nzuri ya kukaa. Nikaona bora nokae karibu na meza moja iliyokuwa imejaa weusi kibao amboa walionekana wakifurahia vinywaji vyao ipasavyo. Nilipoangalia vizuri meza hiyo nikaona kuna kijana ambae niliwahi kuishi nae Malaysia ambae ni Mzenj. Nikamwita na kumkumbusha, kwani alionekana kunisahu. Baada ya kunikumbuka alinikaribisha kwa furaha tele kwenye meza yao. Akanitambulisha kwa rafiki zake, ambapo niligundua kuwa wote ni kutoka Zenj...Baada ya glass mbili hivi nikamuuliza kama kuwa Watz wa bara katika baa hiyo. Akanionyesha kwa kidole kuwa wamekaa kule... Well nikamwambia wacha nikawasalimu nao pia.
Baada ya kukaa kwa Wabongo kwa muda kadhaa nikahisi kuwa kuna kitu kinaendelea kati ya Wazenj na Wabongo... kwani ninapotoka sijawahi kuona utengano wa aina hii. Well sijui ni nani aliyeanzaa. Ila kwa haraka haraka nikahisi kuwa ni Wazenj ambao walikuwa na vituko ambavyo vimepelekea kuwepo na utengano huu... Hata hivyo nitazidi kuchimbachimba ili nijue vituko vyao.....

Thursday 19 April 2007

Uchafuzi wa Mandhari ya Bwawani Hotel

Bwawani Hotel ndio hotel pekee ambayo SMZ inaweza kujisifia kwa namna ilivyojengwa na huduma ambazo zinatolewa na hoteli hiyo. Hotel hii ilijengwa katika miaka ya 70, ikiwa na vyumba 118 kwenye jengo la ghorofa nne. Ipo umbali wa kilometa nane toka uwanja wa ndege na ni mwendo wa dakika tano toka bandarini.

Pamoja na vitu vingine vinavyopatikana katika hotel kubwa, hotel hii ina viwanja wa Tennis ndani na nje, swimming pool ya ndani, ukumbi wa michezo( game room) na bwawa zuri upande wa mbele ya hotel hiyo.

Leo ningependa kuzungumzia juu ya bwawa la hoteli hiyo, ambapo pengine ndio lililo zaa jina la Hotel Bwawani. Bwawa ambalo hadi hoteli inakamilika katika miaka ya sabini, ujenzi wake ulikuwa bado kukamilika, hivyo kuto toa madhari halisi ya hoteli hiyo.

Katika miaka ya themanini, wakati SMZ ikiwa inajichanganya kuamua kufuata mfumo gani wa serikali za mitaa, toka serikali za majimbo, kulijitokeza wawekezaji ambao waliona kuwa upo umuhimu wa kuendeleza bwawa hilo. Katika kipindi hicho tayali madhari ya bwawa hilo ilikuwa ni ya kuchukiza zaidi kuliko kuvutia. Majani maji yalikuwa yakiongezeka kwa kasi kubwa.

Mapendekezo yaliyotolewa na wawekezaji wa miaka hiyo ya themanini ni kuhamisha bandari ya yatch iliyopo kwenye bandari ya Malindi hadi kwenye bwawa hilo, kujenga ofisi ya Meja wa Halmashauri ya Mji wa Zanzibar(Town Hall) katika kingo za bwawa hilo, toka katika Ofisi ya Halmashauri ya Mji katika barabara ya Benjamin Mkapa. Ofisi hiyo ya Meya licha ya kuwa na ukumbi wa mikutano ya Madiwani, pia ungekuwa na club ya yatch zinazotia nanga Kisiwani hapo toka sehemu mbalimbali hapa duniani.

Wazo hili lilipo pelekwa kwenye vyombo vya SMZ lilitupwa kando, licha la kuwa wazo bora kabisa katika kipindi hicho hadi leo na mpaka kesho. Kwani kinachoendelea katika bwawa hilo hivi sasa ni uchafu mtupu. Kwa upande mwingine iwapo wazo hili lingefanyika katika siku zile, matatizo ya kisaikolojia yanayowakuta Madiwani na Meya wao sasa yasingekuwepo. Kuwachanganya Meya na Madiwani wake katika jengo moja na Watendaji wa Manispaa ya Zanzibar kumesababisha kuwepo na miingiliano ya kiutendaji kila siku katika Manispaa hiyo.

Ukiachana na adha za madiwani hao, bwawa hilo ni makaazi ya ndege watokao kaskazini ya dunia wakati wa msimu wa baridi huko kaskazini, hivyo iwapo bwawa hilo lingeendelezwa na kutuzwa vema tungeweza kujifunza mengi kuhusu ndege hao na zaidi kingekuwa ni mojawapo wa kivutio cha utalii. Lakini hili nalo halipo ndani ya mawazo ya watendaji wa SMZ!

Kumekuwepo na mawazo mengi toka serikalini na katika Halmashauri ya Mji juu ya kuendeleza bwawa hilo. Lakini yote kwa upande mmoja ni kuchakaza tu bwala hilo au kuliondoa kabisa.

Katika miaka ya tisini msikiti(Msikiti Mabluu) ambao uliondolewa ili kupisha ujenzi wa bwawa hilo, ulijengwa upya. Ujenzi wa msikiti huo ulikuwa ni kutoa mfano wa mradi mpya wa ujenzi wa nyumba katika muda mfupi. Ujenzi wa msikiti ulikamilika ndani ya siku saba na siku ya nane ukatumika. Mawazo ya ajabu ajabu yakazidi kumiminika, moja wa Mameja alipendekeza kuwa sehemu yenye magugu maji ijazwe kifusi ili kupatikane nafasi ya kuweka makontena ya biashara! Meya mwengine alikuja na wazo kuwa bwawa hilo litumike kuwa jaa kuu la taka.
Pengine waliokuwa wanajitahidi kuliweka bwawa hilo katika hali ya usafi ni wafungwa, ambao kila mwaka kwa mamia hupita hapo kukata magugu maji.

Miaka ya elfu mbili Waziri kiongozi alitoa amri ya wafanyabiashara wa vinyago na batiki wapewe eneo hilo kwa biashara zao, agizo likatekelezwa na madhari ikazidi kuwa mbaya. Hata hivyo kutokana na kuwepo kwa msikiti wauza vinyago walijikuta wakiondolewa hapo.

Ukarabati wa kusuasua wa Bandari ya Malindi umeligeuza tena bwawa hilo kuwa sehemu ya kuhifadhia makontena ya bandarini, hiyo kuendelea kuchafua bwawa na zaidi hata kuziba madhari nzuri ya mbele ya hoteli hiyo. SMZ inadai kuwa uwekaji wa makontena katika eneo hilo ni wa muda tu, na hata bandari itakapokamilika makontena hayo yataondolewa. Cha kujiuliza hapo jee vifusi na michanga iliyojazwa katika bwawa ili kutoa ya uwekaji wa makontena yataondolewa au utakuwa ni mwanzo wa kuzaliwa wazo jingine la kutokomeza bwawa hilo?

Kwa maoni yangu wazo lilitolewa katika miaka ya themanini ya kukamilisha ujenzi wa bwawa na ujenzi wa ofisi ya Meya pembeni ya bwawa hilo, lilikuwa ni wazo pekee ambalo lingeweza kulinusuru bwawa hilo kuwa kichaka cha mawazo duni ya viongozi wa SMZ. Aidha kungesaidia kuendeleza bwawa hilo na kuwa sehemu ya kuvutia kabisa katika eneo la Mji Mkongwe zaidi ya Forodhani.

Wednesday 11 April 2007

Tindikali kwa wauza kilaji Zanzibar

Sijui kisiwa kitaendelea vipi katika sekta ya Utalii kama wauzaji vinywaji vikali wataendelea kuteswa namna hii haya mambo yakuchanganya maswala ya kidini na uchumi hayana maendeleo yoyote Somalia mfano.




Wakala mwingine wa pombe amwagiwa tindikali

2007-04-10 10:28:44
Na Mwinyi Sadallah,Zanzibar

Wakala mwingine wa kusambaza pombe Zanzibar, Bw. Chadalal Javed, amemwagiwa tindikali usoni, muda mfupi baada ya kufungua duka lake lililoko mtaa wa Empire mjini hapa.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi Bw. Bakar Khatib Shaaban alithibitisha kutokea kwa tukio hilo. Tukio hilo lilitokea jana saa 3:00 asubuhi.

Alisema kwamba mfanyabishara huyo mwenye asili ya Asia, alivamiwa na mtu asiyejulikana, muda mfupi baada ya kufungua duka lake.

``Ghafla mfanyabiashara huyo alimwagiwa kemikali na kumjeruhi sehemu za usoni na tayari amepelekwa jijini Dar es Salaam kwa matibabu zaidi,`` alisema Kamanda Bakari.

Alisema kuwa wakati tukio likitokea, mfanyabiashara huyo alikuwa dukani na mkwewe wakijiandaa kutoa huduma kwa wateja wao.

Alisema hata hivyo, polisi hawakufanikiwa kuchukua sampuli za kemikali iliyotumika, kwa vile baada ya tukio kutokea, wahusika waliharibu mabaki ya kemikali hiyo.

Kamanda Bakari alisema kwamba iwapo wangefanikiwa kupata mabaki ya kemikali hiyo, wangeweza kupeleka kwa Mkemia Mkuu kujua aina ya kemikali iliyotumika.

``Hatufahamu, aina ya kemikali iliyotumika,lakini tunaendelea na uchunguzi kwa kuwa mtu aliyefanya uhalifu huo alifanikiwa kukimbia baada ya tukio,`` alisema Kamanda Bakari.

Mfanyabiashara huyo anamiliki duka la Scorch Store, ambalo linatumika kusambaza pombe Zanzibar katika mahoteli ya kitali, baa na watumiaji wa rejareja Zanzibar.

Kamanda Khatib alisema hilo ni tukio la pili kutokea kwa wamiliki wa maduka ya pombe. Alisema mwezi uliopita mfanyabiashara mwenye asili ya Kiasia, Bw. Kirikti Mandala, alimwagiwa tindikali akiwa dukani kwake eneo la Michenzani.

Alisema kwamba katika tukio hilo watu wawili walihojiwa na polisi, lakini hadi sasa hakuna mtu aliyefikishwa Mahakamani kuhusiana na tukio hilo.

Hivi karibuni baadhi ya wanaharakati wa dini, wamekuwa wakilalamika kuongezeka kwa idadi ya baa katika manispaa ya Zanzibar, kitendo ambacho wanasema ni kinyume na mila na utamaduni wa Mzanzibari.

Mwezi uliopita wanaharakati hao, waliandamana kupinga ongezeko hilo la idadi ya baa katika mji wa Zanzibar, lakini hawakutoa takwimu za ongezeko hilo.

* SOURCE: Nipashe

kibunango

Asante kwa kunikaribisha katika blog hii matata yenye jicho katika vihoja vitokeavyo kisiwani Unguja , napenda kwanza kukutakia safari njema uingereza, na vilevile kutoa ahadi yakujitahidi kucompose as many articles as possible tuko pamoja.
Guidance

Safarini Uingereza

Wapenzi wa kona hii ya Vituko vya Zenj, napenda kuwataarifu kuwa nitakuwa safarini Uingereza kuanzia mwishoni mwa wiki hii..

Kwa miezi kadhaa ijayo nitakuwa na blog tokea jiji la London. Zaidi itakuwa jambo la msingi iwapo nitaweza kukutana na wanablog wa Uingereza...na watanzania wengine ambao ni wapenzi wa blog..

Tuesday 6 March 2007

Uchovu wa SMZ kwenye masuala ya Umiliki wa Ardhi...

Moja ya matatizo makubwa ya SMZ yapo kwenye masuala ya umiliki wa ardhi. Serikali hiyo ina migogoro mingi kuhusu umiliki na uendelezaji wa ardhi licha ya kuwa na sheria ya Mipango miji/vijiji na Ardhi ya mwaka 1985, Baraza la Manispaa ya mwaka 1995 na Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe ya mwaka 1994.

Sheria hizo zote hapo juu zinasimamia uendelezaji na umiliki wa ardhi, aidha Halmashauri za wilaya nazo kwa upande mwingine zimekuwa zikisimamia uendelezaji wa ardhi. Serikali kuu kupitia kwa Masheha wao nao wamekuwa wakijishughulisha katika masuala ya ardhi.

Katika Mahakama zote visiwani humo kumejaa kesi nyingi za madai ambazo zinahusiana na matatizo ya ardhi.

Leo kanisa la Anglikana huko Zanzibar limekumbushia kadhia yao ya kunyang'anywa ardhi yao na kufanyia mabadiliko ya matumizi. Kimsingi eneo ambalo lina mgogoro ni shule ya msingi Mkunazini ambayo kabla ya mwaka 1964 ilikuwa inamilikiwa na kanisa hilo.

Kinachoshangaza ni hatua ya SMZ kupitia wizara zake kuendelea kubadilisha kinyamela matumizi ya eneo hilo toka eneo la shule na Ibada kuwa eneo la biashara, kwa kuruhusu ujenzi wa maduka katika eneo hilo.

Miaka ya tisini kanisa hilo liliwahi kuomba ruhusa ya kukarabati uzio wa eneo hilo ambao ulikuwa unazama taratibu. Uzio huo unaanzia upande wa mbele ya shule hiyo mkabala na barabara ya Benjamini Mkapa. Kibali cha ujenzi wa uzio huo kilichukua muda mrefu hadi kupatikana. Na kiliweza kupatikana baada ya kanisa hilo kutoa malalamiko mengi kuhusu urasimu wa vyombo vya SMZ.

Ucheleweshaji wa upatikanaji wa Kibali cha Matengenezo ya Ukuta wakati ule sasa ninaweza kuuelewa vizuri. Inaoneka Watendaji wa SMZ walishaona kuwa eneo hilo linafaa kwa kujengwa kwa Vibanda na Viduka vya biashara hivyo walikuwa wanasita kutoa ruhusa ya matengenezo ya ukuta. Na hata walipotoa ruhusa hiyo eneo lilikuwa karibu na shule hiyo halikupewa ruhusa ya ukarabati.

Sasa eneo hilo limejengwa Vibanda vya biashara, na litaendelea kujengwa licha ya maombi ya kanisa hilo kurejeshewa umiliki wa shule hiyo.

Hivi ni nini nafasi ya kuwa na mamlaka ya hifadhi na uendelezaji wa mji mkongwe, iwapo sehemu ambazo zinahitaji kupatiwa hifadhi kutokana na umuhimu wake wa kihistoria, zinashindwa kuhifadhiwa? Kanisa la Anglikana ni muhimu kabisa katika historia ya Zanzibar. Hivyo linatakiwa lipewe nafasi ya ya kuhifadhiwa chini ya Sheria za Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe.

Thursday 15 February 2007

Sasa ni Disco...!

Katikati ya mwaka jana(2006)SMZ ilipigia marufuku matumizi ya simu za mkononi kwa wanafunzi wote wa shule za Msingi na Sekondari kwa madai kuwa, simu hizo zinachangia kwa kiasi kikubwa kwa wanafunzi kushiriki katika vitendo vya ngono, aidha wanafunzi hao wamekuwa wakipoteza muda mrefu kuandika meseji na kupokea simu wawapo darasani na katika maeneo ya shule.

Sasa SMZ imenyoshea mkono Disco kuwa imesababisha kwa wanafunzi wengi kufeli mtihani wa kidato nne wa mwaka jana. Hivyo ni marufuku kwa mwanafunzi yoyote wa shule ya msingi na sekondari kwenda Disco!

Hatua ya kupiga marufuku kwa wanafunzi kwenda kwenye madisco na kumbi za starehe zimepokelewa kwa mitazamo tofauti na waakazi wa visiwa hivyo, ambapo Disco na mojawapo ya sehemu ndogo tu ya Starehe zinazopatina kwenye visiwa hivyo.

Wanafunzi wengi wanakwenda katika madisco wakati wa sikukuu za Idd ambazo huwa ni mara mbili kwa mwaka, Madisco mengine yanayovuta wanafunzi wengi ni kama tamasha la Mwaka Kogwa ambalo hufanyika mara moja kwa mwaka na Tamasha la nchi za Majahazi. Zaidi wanafunzi huonekana kwenye maonyesho ya Muziki wa Kizazi Kipya. Madisco yote haya hufanyika kuanzia saa za maghalibi hadi usiku wa saa nne.

Katika kuona kuwa wanafunzi wa Visiwa hivyo wanafanya vizuri SMZ imo katika mipango ya kutenganisha wanafunzi kwa kuweka shule za jinsia moja tu. Mpango huu umeshaanzishwa kwa baadhi ya shule visiwani humo kwa lengo la kuwafanya wanafunzi hao wasome na kufaulu na sio kutongozana.

Mwaka jana Visiwa hivyo vilishuhudia amri ya kuwataka wanafunzi wa chuo cha "Zanzibar University College" kutochanganyikana(wanaume na wanawake) wakati wa kujisomea usiku, kwa madai kuwa chuo kimezagaa na kondomu zilizotumika!

Hatua za SMZ kutaka kuona kunakuwepo na matokeo mazuri ya mitihani kwa wanafunzi wake zichukuliwe kufuatana na mapendekezo kadhaa yaliyokwisha kutolewa huko nyuma. Kwanza SMZ imekwisha shauriwa mara kadhaa kuhusu kubadilisha mitaala yake ili iendane na ya Tanzania bara. Hata hivyo hadi sasa SMZ wanaonekana kuwa bado kuwa tayali kufuta pendekezo hilo, licha ya kujua manufaa yake kwa wanafunzi na wanakisiwa hicho kwa ujumla. Kinacho zuia kutofuatwa kwa pendekezo hilo hadi leo hakijulikani. Zaidi ni kwa serikali hiyo kuibuka na viamri vya ajabu ajabu kila kukicha! Kitendo cha kupiga marufuku marufuku hizi husababisha kuwafanya wanafunzi kuwa watukutu zaidi.

Kwa upande mwingine Wazazi nao wanapaswa kushirikishwa katika kila hatua ya maendeleo ya wanafunzi wanapokuwa shuleni na majumbani. SMZ inapaswa kushirikiana na wazazi kuona ni kwa kiwango gani wataweza kuongeza bidii ya wanafunzi katika masomo yao. Malezi bora kwa mwanafunzi husaidia kwa kiasi kikubwa kwa mwanafunzi kuwa na bidii katika masomo yake.

UNCEF wanathibitisha hilo kwa kuwa hata nchi zenye utajili mkubwa iwapo wanafunzi wake wanakosa malezi bora matokeo ni kufanya vibaya shuleni.

http://news.bbc.co.uk/2/hi/uk_news/6359363.stm

Tuesday 23 January 2007

Nungwi : Ukahaba, Nguo fupi na Ulevi hauna nafasi..

Linapokuja suala la ukahaba, Kijiji cha Nungwi huko Zanzibar kimekuwa mbele kukanya tabia hizo wazi wazi. Wamejaribu kutumia njia mbalimbali ikimemo maandamano, risala na kutimia viongozi wao katika kukemea tabia hiyo, hali hiyo ni tofauti kidogo na mjini Zanzibar ambapo makundi ya vijana hujichukulia sheria mkononi kuwahadhibu makahaba na wale wavao nguo fupi.
Hatua iliyochukuliwa mwanzoni mwa wiki hii na Kamati ya Maadili na Maendeleo katika kijiji cha Nungwi ya kutunga sheria ndogo ya kudhibithi uvaaji nguo fupi, ukahaba na ulevi inathibitisha ni kwa jinsi gani wanakijiji hicho hupenda kupita katika njia zinazokubalika katika kutoa kero zao.
Nikirudi nyuma na kuangalia kile kinachodaiwa kuwa ni ukahaba na mambo mengine yanayokwenda tofauti na maadili ya wakaazi wa Nungwi, yalianza mara baada ya kijiji hicho kukaribisha hoteli za kitalii. Kabla ya kuja kwa hoteli za kitalii kijiji hicho kilikuwa ni maarufu kwa uundaji wa majahazi na shughuli za uvuvi.
Miaka ya tisini ambayo ilikuwa ni ya mabadiliko makubwa katika sekta ya utalii visiwani huko, Waakazi wa Nungwi walishuhudia maandamo ya kinamama kupinga kuwepo kwa wanawake na wasichana toka mkoani Tanga ambao walidaiwa kuwepo huko kwa lengo la kufanya ukahaba. Wakinamama hao walidai wadada hao toka Tanga wamekuwa wakiwarubuni waume zao na kufanya nao mapenzi kwa pesa na kusababisha hali ngumu katika nyumba zao. Waliendelea kwa kusema uwepo wao hapo kutasababisha kuongezeka kwa ukimwi na kupolomoka kwa maadili. Hivyo waliwataka akinadada hao kuondoka mara moja kijijini mwao. Hatua yao hiyo ambayo iliungwa mkono na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini, ilizusha mjadala mrefu kuhusu nafasi ya Wabara katika visiwa hivyo. Zaidi ilionekana kuwa Watz bara wanazuiwa kutumia haki yao ya msingi ya kwenda popote pale ndani ya Tanzania pasipo bughuza. Hata hivyo maandamano hayo yalishuhudia kuongezeka kwa Watanga ambao sasa walihamia mjini na vijiji vingine vyenye hoteli za kitalii.
Nungwi hawakuishia hapo, wakanyosha vidole kwa wageni wengine ambao ni wafanyakazi wa mahoteli kwamba wanavaa nguo fupi na suruali za kubana. Kipindi hicho wafanyakazi wengi katika hoteli za kitalii huko walikuwa ni wananchi toka Kenya.
Hatua za Kamati hiyo ya kutunga sheria ndogo ndogo za kudhibiti uvaaji wa nguo fupi na ukahaba, ni hatua nzuri katika kulinda maadili yao. Hata hivyo kuna vitu kadhaa vya kujiuliza juu ya uhalali wa sheria hizo ndogo ndogo na hasa katika kuzisimamia na utekelezaji wake. Kimsingi kuhusu uvaaji wa nguo fupi, kamati hiyo inawataka wale wote wavaao nguo fupi kuvaa vazi la Kizanzibari. Vazi la kizanzibari kwa ufahamu wangu ni kuvaa kanga zaidi ya mbili, huku ukiwa umefunika sehemu zote za mwili na kuachia sura tu. Sheria hii inaweza isikubalike kwa wengi wa wafanyakazi katika hoteli hizo ambao sio wenyeji wa zanzibar.
Na iwapo vazi la kizanzibari ni kama lile la kuvaa baibui na hijabu yake, basi sheria hiyo itakuwa inalenga zaidi maadili ya kidini kuliko maadili ya kizanzibari, na itakuwa sio kosa kuhoji kauli ya serikali ya kusema kuwa nchi hiyo si ya kidini. Na kwanini wananchi ambao sio wa dini fulani washurutishwe kuvaa baibui?
Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kaskazini ambayo ndio imepelekewa sheria hizo ili izibaliki, kabla ya Sheha na Wajumbe wake kuanza kucharaza viboko hadharani kwa dada zetu, itabidi iipitie vizuri sheria hizo kabla ya kuziruhusu kutumika. Lengo ni kuona haki sawa kwa waakazi wa kijiji hicho na kisiwa cha zanzibar kwa ujumla, inazingatiwa.

Sunday 21 January 2007

Mstakabala wa Soko la Usiku....

Wengine wamediriki kusema ni mojawapo wa kivutio cha watalii wawepo Zanzibar, huku wengine wakisema ni sehemu nzuri ya kwenda jioni iwapo huitaji kupika, na vijana wakipasha kuwa ni sehemu nzuri ya kukutana na marafiki wapya! Hiyo sio sehemu nyingine yoyote bali ni bustani ya Forodhani. Soko la chakula na vinywaji baridi wakati wa usiku.
Kwa miaka mingi eneo la bustani ya Forodhani limekuwa likitumika kwa shughuli mbalimbali, ikiwemo ya soko la lachakula kuanzia jioni hadi usiku. Jioni eneo hilo hilo hutumika kwa ajili ya michezo hasa mpira wa miguu na kuogelea. Muda wa maghahalibi ukifika eneo hilo hugeuka na kuwa soko. Miaka ya karibuni matumizi katika eneo hilo yamezidi kuongezeka, siku hizi asubuhi hadi usiku eneo hilo hutumika na wauza vinyago na batiki. sehemu nyingine hutumika kwa madereva kupumzika wakati wakisubiri wateja wao... hasa watalii.
Upanukaji wa matumizi ya eneo hilo kumeleta uharibifu mkubwa wa mazingira ya bustani hiyo. Aidha wingi wa watu watumiao bustani hiyo umezidi sana kiasi cha bustani hiyo ya Forodhani kuchakaa kwa kasi kubwa. Pamoja na kuzidiwa huko na wingi wa watumiaji bustani hiyo imeendelea kutumika kwa shughuli kupishana kutokana na muda wa siku, yaani asubuhi eneo linatumika hivi, mchana vile na usiku namna hii. Na inapotekea shughuli maalumu basi hutavutiwa muda muufaka ili isije kera shughuli zingine, na hasa soko la chakula....!
Uharibifu wa kwanza kuonekana katika bustani hiyo, ulitokana na wauzaji wa vyakula katika eneo hilo kuanza kupika ndani ya bustani. Hali ya bustani ikawa ni mbaya sana, hadi kufikia kufungwa. Baada ya kuafikiana na Manispaa ya Zanzibar, wafanyabiashara wa usiku walikubali kurejea mtindo wao wa awali wa kutopika katika bustani. Zaidi ni kuja na vyakula ambavyo vimekwisha pikwa tokea majumbani mwao. Tatizo lao likawa limepatiwa dawa.
Kwenye mikusanyiko ya watu hapakosi kadhia zake, wenye vipando hasa pikipiki, vespa na magari madogo, wakaona ni vema kuingia na vyombo vyao ndani ya bustani hiyo. Sijui ni nini hasa kilichopelekea watu hao kufanya hivyo. Vijia ndani ya bustani ambavyo vilikuwa ni maalumu kwa watembeao kwa miguu vikavamiwa na vyombo, haikuchukua muda navyo vikachoka. Mamlaka kama kawaida ikachukua hatua. Mara hii ikawa ni kuvipiga marufuku vyombo vyote ndani ya bustani.
Uchovu wa bustani hiyo sasa ukawa upo wazi kwa kila mtu kuuona, pasipo kujali kama ni mtaalamu au la.. Wanjanja vilevile wakaona hilo huku wakijua mapungufu ya mamlaka husika katika kutengeneza bustani hiyo. Wajanja hao wakatoa masharti yao ili kuweza kurejesha madhali nzuri ya bustani hiyo, ambayo sasa ilikuwa ni mojawapo ya vivutio vya utalii katika kisiwa cha Zanzibar. Sharti lao kubwa walitaka wapewe eneo la kufanyia biashara ndani ya bustani hiyo, aina ya biashara yao ni mgahawa. Bila ajizi Mamlaka husika wakatoa nafasi, Mgahawa ukajengwa na bustani ikafanyiwa matengenezo kidogo sana. Mgahawa ukashamiri na bustani ikaendelea kuharibika.
Bustani hiyo ina bahati ya kusimamiwa na zaidi ya Idara tatu kubwa za serikali, Kuna Manispaa ya Zanzibar, ipo Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe na Idara ya Mipango Miji. Mamlaka hizi zote zimekuwa zikishindana katika kusimamia bustani hiyo, na hasa linapokuja suala la uendelezaji wa bustani hiyo. Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji Miji Mkongwe, chini ya sheria ya mwaka 1994, imekuwa ikidai ndie muhusika mkuu, huku Manispaa chini ya sheria ya mwaka 1995 nayo ikidai inapaswa kusimamia eneo hilo. Idara ya Mipango miji ikiendelea kutumia sheria yake ya mwaka 1985, imekuwa ikitaka kuhusishwa kwa kila kitu ndani ya bustani hiyo.
Idara hizo kila mmoja kwa wakati wake ilijaribu kupanga ni kwa namna gani eneo hilo litaweza kurudishwa katika hali yake hasa kimazingira. Manispaa kupitia Mpango wa Mji Endelevu waliona ni vema kufanyia matengenezo bustani hiyo. Lengo kubwa la Mji endelevu ni kuwashirika wadau wote wa bustani hiyo katika matengenezo ya bustani. Hii ni kwa sababu waliamini kwa kuwashirikisha wadau patakuwepo na uendelevu wa bustani. Mamlaka ya hifadhi na uendelezaji wao walikubaliana na Agha Khan kuifanyia matengenezo bustani hiyo na zaidi kuipanua. Wakati taasisi hizi mbili zikijadili nani afanye matengenezo, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ikaibuka na ufadhili toka kwa asasi ya Mke wa Rais wa Zanzibar(Karume) kuwa wapo tayali kuanza kuifanyia matengenezo bustani hiyo, chini ya maelekezo ya Manispaa.
Mamlaka ya hifadhi na uendelezaji mji mkongwe, wakaona iwapo watabariki matengenezo hayo watakuwa wanakwenda kinyume na Agha Khan, ambao wanampango wa muda mrefu wa kutengeneza bustani hiyo na kisha kuigawa upya. Hivyo wakashindwa kutoa idhini ya matengenezo. Manispaa ambao hukusanya mapato katika eneo hilo, wakaanza kufanya matengenezo kwa kasi ya konokono kupitia mfuko wa Mji endelevu, huku wakisikilizia ni nani ambae atapewa baraka zote kati ya Agha khan na asasi ya mke wa rais.
Hayo yakiendelea kwa upande wangu napenda kuwashauri kuwa uwamuzi wowote ambao utatolewa basi uwashirikishe moja kwa moja wadau wa eneo hilo. Matengenezo hayo yawe ni kwa faida ya wadau wa eneo, ambao wapo hapo kila siku. Na iwapo watashirikishwa katika matengenezo na kuhakikishiwa kuendelea kufanya biashara katika bustani hiyo, watakuwa na uchungu iwapo wataona bustani hiyo itaharibika, kwani kwa kushiriki kwao katika matengenezo ni njia mojawapo ya kuwafanya waithamini eneo hilo na kulienzi.

Thursday 18 January 2007

SMZ yafanya kweli

Kwa muda mrefu mifuko ya plastic nyepesi imekuwa ikitumika kwa wingi katika visiwa vya Zanzibar, kuja kwa mifuko hiyo kulitokana na kisiwa hicho kuwa kivutio cha pekee cha biashara katika afrika ya mashariki katika ile miaka ya tisini mwanzoni... Matumizi ya mifuko hiyo ilikuwa ni kwa bidhaa mbalimbali, aidha mteja hakupaswa kulipia chochote kwa ajili ya bidhaa yake kutiwa ndani ya mifuko hiyo.
Umaarufu wa mifuko hiyo ikashika kasi kiasi kwamba ikiwa sio lazima tena kwenda sokoni au dukani ukiwa na kikapu au mkoba. Umaarufu huo ukaongezeka hadi kufikia kwenye vyakula, sasa ikawa ukienda kununua mbatata za urojo huna haja ya kwenda na chombo chako kwani mifuko ya plastiki ipo. Ukishindwa kumaliza biriani yako hotelini, huna shaka kwani mifuko ya plastiki ipo, iwapo chakula kwenye sherehe au shughuli za misiba kikabaki na ukataka kwenda nacho nyumbani, mifuko ya plastiki ilikuwa ni karibu kuliko chombo chochote kile.
Wenye kuishi kwenye nyumba za ghorofa nao wakaja na udhuru wao, kuwa maji ni ya shida na kamwe hajafiki kwenye ghorofa zao! hivyo kuwafanya wapate shida kubwa linapokuja suala la kujisaidia iwe haja kubwa au ndogo. Njia mbadala ya karibu ikawa ni kutumia mifuko hiyo ya plastiki kukamilisha haja zao, na baade kuitupa chini.
Watumiao vyombo vya moto nao hawakuwa nyuma katika kutumia mifuko hiyo. Chombo kiliendeshwa hadi kwisha mafuta, baada ya hapo mtu hukimbilia kituo cha kuuzia mafuta na mfuko wake wa plastiki. Baada ya kuuziwa mafuta ya kuyatia chomboni mfuko hulembewa mbali pasipo kujali lolote.
Miaka ikaenda na ustawi wa mifuko ya plastiki ukashamiri, sasa ikawa kila baada ya hatua mbili utembeapo kwa miguu unakanyaga mifuko iliotupwa ya plastiki. Bustani, baraza na viunga vyote vikajaa uchafu wa mifuko ya plastiki. Kelele za mji kuwa mchafu zikapamba moto na Halmashauri ya Mji ikaonekana haifanyi kazi yake ipasavyo.
Serikali ikaliona hilo, semina, kongamano na warsha zikafanyika ili kujua athari za mifuko hiyo, Halmashauri kwa upande wake ikatunga sheria ndogo ya kudhibiti matumizi ya mifuko, ambayo haikuwahi kufanya kazi hata siku moja.
Baada ya miaka kumi na ushee sasa, serikali imeona na kuamua kulivalia njuga tatizo la mifuko ya plastiki nyepesi, na ni baada ya kuja na sheria kali dhidi ya matumizi ya mifuko hiyo. Ikiwa ni pamoja na kutumikia kifungu cha miezi sita jela au faini ya dola za kimarekani 2000.00.
Matumizi ya mifuko hiyo kwa zaidi ya miaka kumi kumesababisha uharibifu mkubwa wa mazingira ya kisiwa hicho pamoja na bahari ya Hindi. Ikumbukwe kuwa Taka maji ambazo huchanganyika na mifuko hiyo humwagwa kwenye bahari pasipo kuwepo na mchujo wowote ule, hivyo kuwepo na uharibifu wa maisha katika bahari.
Wafanyabiashara kwa upande mmoja wamekuwa mstari wa mbele kupinga kupigwa marufuku kwa utumiaji wa mifuko mepesi ya plastiki kwa kigezo cha serikali kupoteza mapato ilhali mazingira yakitetekemea. Uwamuzi wa serikali ni wa kuungwa mkono kwa dhati kuanzia kwa wananchi hadi kwa wafanyabiashara, kwani unalengo muhimu wa kuhifadhi na kutunza mazingira ya kisiwa chetu!

Tuesday 9 January 2007

Alijenga Baba na kamalizia Mtoto

Leo Wazenj na Watz wanasherekea siku ya Mapinduzi ya Zanzibar ukiwa ni mwaka wa 43. Mapinduzi hayo ambayo lengo lake kubwa ilikuwa kuwapa weusi wengi madaraka ya kujitalawa.

Tokea Mapinduzi kumeshapita awamu zaidi ya sita za uongozi wa ngazi ya juu kabisa visiwani humo, nikiwa na maana marais wa serikali ya mapinduzi, maarufu kama SMZ. Kila awamu iliingia na mambo yake waliyoona ni muhimu kwa wakati wao, zaidi kila awamu inakumbukwa kwa mazuri na mabaya waliyofanya.

Awamu ya kwanza ilikuwa na lengo la kuwawezesha wananchi walio wengi kuwa na maisha bora. Na hii ilithibitishwa na ujenzi wa nyumba bora katika kila pande ya kisiwa hicho. Juhudi za ujenzi huo zilifanyika kwa pamoja kati ya serikali na wananchi. Yaani wote walishiriki kikamilifu katika ujenzi wa nyumba tena wakitumia kila kitu katika kufanikisha azma ya serikali kuwapatia maakazi bora. Utaratibu uliotumika ni kuvunja nyumba ndogo ndogo zilizojengwa kiholela na kujenga nyumba kubwa za ghorofa. Mfano ni majengo ya Forodhani. Kwa upande mwingine nchi za ulaya nazo hazikuwa nyuma kuona wakaazi wa kisiwa hicho wananufaika, Ujerumani nao wakajenga nyumba za maendeleo katika mtaa wa Kikwajuni ambazo zilikuwa na kila kitu ambacho kinahitajika kwa maisha bora.

Awamu iliyofuata ikaona ni vema kuwa na nyumba nzuri vijijini vilevile, hivyo nayo ikajikita katika kujenga nyumba za vijiji huku wao wakitoa mafundi na vifaa vya ujenzi na wananchi wakifyatua matofali. Vijiji vikajengwa na wananchi wakahamia.

Awamu mbili zikapita pasipo kujishughulisha kabisa na masuala ya ujenzi wa nyumba, licha ya kuwepo na matatizo na kasoro nyingi katika ujenzi wa nyumba katika awamu zilizopita. Mojawapo ya matatizo ni kutomalizika kwa ujenzi wa Nyumba za Michenzani na baadhi ya nyumba za vijiji kukosa wakaazi. Aidha matatizo mabaya ya matumizi ya nyumba hizo na uchakavu wa nyumba. Mbaya zaidi ni kwa wale ambao walivunjiwa vibanda vyao kupisha majengo hayo waliendelea kusota pasipo kujua ni lini watanufaika na nyumba bora.

Awamu ya tano iliingia na aina mpya ya ujenzi wa nyumba, ambao uliitwa nyumba za mkopo nafuu, lengo likiwa ni ujenzi wa nyumba za kisasa kwa kuwauzia wananchi hasa wafanyakazi wa SMZ ambao wengi wao walikuwa hawana nyumba. Serikali ya Uchina ikajitutumua na kujenga nyumba za mkopo nafuu. Kasheshe ikaanza wakati wa ugawaji wa nyumba hizo, malengo yakapindishwa na waliopata wakapata na waliokosa wakakosa, malalamiko yakazidi na serikali kama kawaida yake ikaendelea kutoa ahadi kuwa zitajengwa zingine. Zaidi awamu hii ikachungulia na kule kwenye mabaki ya ujenzi wa nyumba za Michenzani. Wakajipanga na kumalizia block moja, wanainchi wakapata nyumba, kama vile haitoshi kukawepo na malalamiko kuwa nyumba nyingi wamepewa watu toka kisiwa cha pili.

Kuingia kwa awamu ya sita kukabadili kidogo sura ya ujenzi wa nyumba, wao wakaona ni bora kumalizia majengo ya Michenzani na kuwapa wale waliovunjiwa nyumba zao karibu miaka therathini na ushee! Wakawata watu hao kuwa wavumilivu kwani serikali haina fedha za kutosha ila nyumba zitamaliziwa.
Hapa sio kama zamani ambapo wananchi walishiriki ujenzi wa nyumba hizo. Sasa ikawa ni kazi ya serikali pekee kumalizia nyumba hizo. Pengine wananchi walishachoka kuisaidia serikali yao. Sijui.

Umaliziaji wa nyumba za Michenzani utakuwa ni furaha ya pekee kwa Rais Aman Abeid Karume. Kwani nyumba hizo zilijengwa na baba yake ambae alikuwa ndio rais wa kwanza wa SMZ. Pengine Karume ameshawishika kumalizia nyumba hizo ili kukamilisha ndoto za baba yake ambae alitaka kuona kuwa wananchi wake wanaishi katika nyumba zilizo bora kabisa. Aidha ni kuondoa kero za wale ambao walivunjiwa nyumba zao kwa mategemo ya kuishi kwenye nyumba bora, na kujikuta wakisubiri kwa zaidi ya miaka arobaini.

Mwisho napenda kuipongeza SMZ kwa kufikisha miaka 43.