Tuesday 4 October 2016

Ashauri Mahari Ilipiwe Kodi ...



MWALIMU wa somo la biashara katika skuli ya sekondari ya Chasasa Wete Pemba Ali Hamad Nondo, amezishauri Mamlaka ya Mapato Tanzania ‘TRA’ na Bodi ya Mapato Zanzibar ‘ZRB’ kuchukua kiwango cha fedha (VAT) kwenye vyeti vya ndoa, ikiwa ni njia nyengine ya kukuza pato la taifa.

Alisema hata mahari nayo yamekuwa yakipanda siku hadi siku, na wakati wa kufungishwa kwa sunna hiyo, hutolewa cheti cha ndoa baada ya maharia kulipwa, hivyo ni yema kukawa na kiwango cha fedha kinachoingia serikalini.

Mwalimu huyo, ametoa ushauri huo alipokuwa akichangia mada kadhaa kwenye semina ya siku moja ya kuelezea umuhimu wa kulipa kodi, kwa wanafunzi na waalimu wa skuli hiyo.

Alisema kama bado TRA na ZRB hawachukua ‘VAT’ kwenye cheti cha ndo, wakati umefika sasa kufanya hivyo, maana kwenye taratibu hizo huwepo kwa cheti cha ndoa kutoka mamlaka za kiserikali.

“Mimi nauliza kwenye cheti cha ndoa kuna VAT, kama jawabu hakuna sasa anzisheni hiyo, ili mfuko wa serikali ukuwe, maana nayo mahari yanapanda kila siku’’,alishauri.

Akijubu hoja hiyo, Afisa Uhusiano wa Bodi ya Mapato Zanzibar ‘ZRB’ Khamis Makame Mohamed, alisema kwa sasa wao hawakusanyi hata shilingi moja kwenye cheti cha ndoa, ili kama jamii ikiridhia ni jambo jema.

“Hili ni jambo jema, sisi tutalichukua na kulifikisha kwa wenzetu, lakini kwa sasa pamoja na mahari kuonekana kupanda juu, lakini hatuna kodi, maana kwanza ni jambo la kiimani linataka ufafanuzi wa kina”,alieleza.

Nae Afisa Elimu kwa walipa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA ofisi ya Zanzibar, Saleh Haji Pandu, alisema kwa sasa mamlaka hiyo, inakusanya ushuru wa forodha na kodi ya mapato pekee na wala sio kwenye cheti cha ndoa.

Mapema akizungumza kwenye semina hiyo, Afis huyo wa elimu kwa walipa kodi, aliwataka wanafunzi na waalimu hao kuwa wa mwanzo kuwadai risiti za bidhaa wafanya biashara mara wapato huduma.

“Nyinyi muwe mabalozi kwa wafanyabiashara kwamba mkishanunua bidhaa msisite kuwataka wawape risiti, maana kama hakutoa huyo ni ehemu ya kukwep kuliopa kodi.

Wakichangia mada kadhaa kwenye semina hiyo, washiriki hao walipendekeza iwepo taasisi moja pekee ya kukusanya kodi ili kuwapungizi usumbufu wafanyabiashara.

Mwanafunzi Yasseir Hamad Ali, alisema itakuwa jambo la busara kama kutakuwa na chombo kimoja cha kukusanya kodi ili iwarahisishie wanaopaswa kulipa kodi moja kwa moja.

Semina kama hiyo juzi walifanyiwa waandishi wa habari na wafanyabiashara kwa lengo la kukuza uwelewa wa ulipaji kodi kupitia TRA na ZRB.
………………………………..

Sunday 14 August 2016

TANZIA : Mzee Aboud Jumbe amefariki dunia



Rais wa pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mzee Aboud Jumbe amefariki dunia leo hii.

Marehemu alizaliwa tarehe 14.06.1920.

Marehemu alikuwa Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar tokea mwaka 1972 hadi 1984.

Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi.

Sunday 26 June 2016

Mv Happy yazama karibu na Kisiwa cha Chumbe....



Meli ya mizigo iitwayo Happy ikitokea Dar es salaam kwenda Zanzibar imezama eneo la Chumbe, Unguja.

Taarifa zimedai kwamba Meli hiyo ilianza kuzama saa 10 alfajiri baada ya kuingiza maji ndani na kukosekana kwa vifaa kama motor ya kutolea maji hayo kufikia saa 1 asubuhi hii Meli hiyo ilizama kabisa ndani ya maji.


Meli hiyo ilikuwa imebeba Dengu gunia 450 pamoja na Mbao zaidi ya 1000 huku wafanyakazi sita waliokuwa ndani ya Meli hiyo wakiokolewa.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa ni meli ya mizigo mitupu na mabaharia mpaka sasa imeripotiwa kwamba wote ni wazima.


Source: Jamiiforums

Wednesday 1 June 2016

Zanzibar's pioneering pension scheme.....



Tanzania’s semi-autonomous archipelago of Zanzibar has introduced a pension scheme for all citizens aged 70 and over.

It is the first fully funded state pension in East Africa.

Each pensioner will be entitled to 20,000 Tanzanian shillings ($9, £6) a month.

Campaigners have welcomed the move and say it will lead to a huge improvement, not just in the lives of the elderly - considered to be among the poorest in society - but for the rest of the country as well.

Source:

BBC Africa.

Tuesday 31 May 2016

Ulinzi Mkali Leo Kuelekea Polisi Ziwani...



Ni baada ya Maalim Seif kutakiwa kufika Polisi kwa kuhojiwa.

Wednesday 18 May 2016